NAFASI ZA KAZI WIZARA YA MALIASILI NA UTALII 13-10-2021


Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Katibu Mkuu, Wizara

ya Maliasili na Utalii anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa na

uwezo wa kujaza nafasi Mbili (02) kama zilivyoainishwa katika tangazo hili.

AFISA UFUGAJI NYUKI DARAJA LA II - (NAFASI 1)

MAJUKUMU YA KAZI

i. Kusimamia uanzishaji wa hifadhi za nyuki na manzuki;

ii. Kutangaza Sera na Sheria za ufungaji nyuki;

iii. Kufundisha masomo ya fani ya ufugaji nyuki;

iv. Kukusanya takwimu za rasilimali na ufugaji nyuki;

v. Kupanga na kupima ubora wa mazao ya nyuki; na

vi. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na Msimamizi wa kazi.

Kuajiriwa wenye Shahada katika moja ya fani zifuatazo, Ufugaji Nyuki, Sayansi ya Elimu

ya Mimea, Elimu ya Wadudu au Elimu ya Wanyama kutoka Chuo Kikuu cha Dar es

Salaam au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

MSHAHARA

Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS D.

  AFISA WANYAMAPORI DARAJA LA II- (NAFASI 1)

i. Kutekeleza kazi za ushirikishaji wadau katika uhifadhi;

ii. Kudhibiti utoaji wa leseni za biashara ya nyara na vibali vya kukamata

wanyama hai;

iii. Kushiriki katika kusuluhisha migogoro ya matumizi ya wanyamapori;

iv. Kudhibiti matumizi haramu ya leseni za uwindaji na kuhakikisha kufuatwa kwa

maadili katika kutumia wanyamapori;

v. Kudhibiti matumizi haramu ya wanyamapori;

vi. Kufuatilia utekelezaji wa miongozo mbalimbali ya uhifadhi wanyamapori;

vii. Kuhakiki viwango vya kukamata wanyama hai kwa ajili ya biashara na ufugaji;

viii. Kufanya kazi za kuzuia ujangili;

ix. Kukusanya taarifa na takwimu za Uhifadhi;

x. Kutekeleza kazi za uhifadhi katika Mapori ya Akiba; na

xi. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na Msimamizi wa kazi.

 SIFA ZA MWOMBAJI

Kuajiriwa wenye Shahada ya Sayansi ya Wanyamapori kutoka Chuo Kikuu

kinachotambuliwa na Serikali.

MSHAHARA

Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS D.

 

MASHARITI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.

i. Waombaji wote wawe ni raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45.

ii. Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.

iii. Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za

kuingilia katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za

maombi ya nafasi za kazi kwa Waajiri wao na Waajiri wajiridhishe

ipasavyo.

iv. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Wasifu Binafsi)

yenye anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini

watatu wa kuaminika.

v. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya

kidato cha nne na kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti

vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.

- Cheti cha Shahada ya Uzamili/Shahada/Diploma ya Juu/

Diploma/Cheti.

- Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI

- Cheti cha mafunzo ya Kompyuta

- Vyeti vya kitaaluma kutoka katika Bodi husika

vi. Vyeti vya ushiriki wa mafunzo (Testimonials), Hati za matokeo ya mafunzo

za muda (Provisional Results), Taarifa za Matokeo (Statement of results),

Hati za matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI

RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.

vii. Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao

vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (Tume ya Vyuo Vikuu

Tanzania (TCU), Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) na Baraza la Taifa

la Elimu ya Ufundi (NACTE).

viii. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba

isipokuwa kama wana kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.

ix. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko

katika Utumishi wa umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo

yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba,2010.

x. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za

kisheria.

xi. Mwisho wa kutuma maombi ya kazi ni tarehe 26, Oktoba, 2021.

Muhimu, kumbuka kuambatisha barua yako ya maombi ya kazi iliyosainiwapamoja

na vyeti vya elimu. anuani ya barua hiyo ielekezwe kwa;

 

Maombi yote yatumwe kwenye mfumo wa kielektroniki wa Ajira (Recruitment Portal) kupitia anuani ifuatayo; http://portal.ajira.go.tz/


Comments

Popular posts from this blog

22 Characteristics of Entrepreneurs

Writing your business plan summary

Secrets of Successful Forex Traders